ADSENSE FLOAT CENTER

Wednesday 25 April 2018

Polisi Yatoa Onyo Kali kwa Watakaoandamana Kesho " Tumejipanga Hakuna Maandamano Yatakayofanyika Kesho"

Polisi Yatoa Onyo Kali kwa Watakaoandamana Kesho " Tumejipanga Hakuna Maandamano Yatakayofanyika Kesho"
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewataka wananchi wote kuendelea na shughuli zao kama kawaida kwa kuwa maandamano yanayozungumzwa hayapo na ni batili.

Akizungumza leo Jumatano Aprili 25 na shirikisho la waendesha bodaboda Mkoa wa Dar es Salaam, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, ACP Sweethbert Njwele amesema jeshi la polisi limejipanga kuhakikisha kila mtu anafanya shughuli zake kama kawaida bila uvunjifu wowote wa amani.

"Niwahakikishie jeshi la polisi tumejipanga na mkoa wetu utaendelea kubaki salama hakuna maandamano yatakayofanyika hivyo kila mtu aendelee na shughuli zake kama kawaida," amesema Njwele.

Amesema waendesha bodaboda ni kundi kubwa ila kuna baadhi yao si waaminifu na kutaka wajiepushe na watu watakaowashawishi kuvunja sheria za nchi.

Kwa upande wake, Msemaji wa Shirikisho hilo Adamu Kyando amesema uvumi unaosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Aprili 26 bodaboda watashiriki si kweli kwani hakuna bodaboda yeyote atakayeshiriki maandamano hayo.

"Kuna taarifa zinazosambaa kwenye mitandao yakijamii ikihamasisha bodaboda kushiriki maandamano taarifa hizi si za kweli na ni batili," amesema Kyando.

Amesema kwa yeyote atakayeshiriki maandamano hayo uongozi hautahusika kwani taarifa zinazosambazwa hazitoki kwenye shirikisho hilo. 

Install Application ya Udaku Special Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi
=>BOFYA HAPA KUINSTALL/DOWNLOAD

Sunday 7 January 2018

Nay wa Mitego Ahamishiwa Sentro Dar, Huenda Akapandishwa Mahakamani!

DAR ES SALAAM: Rapper Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ jana jioni alihamishiwa katika Kituo cha Kikuu cha Polisi (Sentro) jijini Dar es Salaam kutoka Mvomero, Morogoro alikokuwa anashikiliwa na polisi kuanzia asubuhi ya Jumapili, Machi 26 kutokana na kuachia wimbo unaodaiwa kuwa una maneno ya kichochezi na kuikashfu serikali iliyoko madarakani.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Wakili Peter Kibatala aliandika;

Taarifa nyingine zimeeleza kuwa, Wakili Peter Kibatala naye amejitolea kumtetea bure Nay wa Mitego endapo atapandishwa mahakamani.

Awali, taarifa ya Jeshi la Polisi mkoani Morogoro ilieleza kuwa walianza kumsaka Nay wa Mitego baada ya kuarifiwa kuwa ametimkia, Dodoma, na baada ya kumkamata walitakiwa kumrudisha Dar es Salaam ambako niko lipo shauri la kesi yake.
Kwa upande wao Baraza la Sanaa Tanzania, BASATA wamedai kuwa wimbo alioutoa Nay hivi karibuni ‘WAPO’ hauna maadili na una maneno ya kichozchezi

USILO LIJUA KUHUSU NANDY

KATIKA pasipoti yake ya kusafiria anatambulika kwa jina la Faustina Charles lakini kwa mashabiki wa Muziki wa Bongo Fleva wanamtambua kama Nandy a.k.a African Princess.
Anafanya poa katika Muziki wa Bongo Fleva kwa sasa ambapo ukiongelea miongoni mwa wasanii wa kike waliopo kwenye chati kwa sasa huwezi kumuacha. Ngoma iliyomtambulisha ilikuwa ni Nagusa Gusa ambayo remix yake amemshirikisha Mr.Blue.
Over Ze Weekend limekuwekea kwa ufupi baadhi ya mambo usiyoyajua kuhusiana na Nandy anayebamba kwa sasa na Ngoma ya Wasikudanganye.
Alikataa kuishi Nigeria
Alikuwa mshindi wa kwanza katika Shindano la Karaoke Barani Afrika la Tecno Own The Stage lililofanyika Februari 2016 nchini Nigeria.
Katika shindano hilo, Nandy aliibuka nafasi ya pili na kujizolea shilingi milioni 36 pia kuahidiwa kuingia katika lebo kubwa nchini Nigeria ya Chocolate City na kufanya kazi huko lakini alikataa na kujiunga na Jumba la Vipaji (THT) ambao yupo nao hadi sasa.

Nandy.
Anawavalisha mastaa
Nje ya muziki, Nandy ni bonge dizaina kwa mastaa…mavazi yake yote anayoonekana amevaa ya asili huwa anabuni mwenyewe na kushona.
Miongoni mwa watu maarufu aliowahi kula shavu la kuwa-bunia baadhi ya mavazi hayo ni Naibu Spika Dk. Tulia Ackson.
Milioni 36 zamtoa
Kati ya vitu anavyojivunia kupitia kipaji chake ni pale alipokuwa mshindi wa pili katika shindano hilo la Karaoke na kujipatia shilingi milioni 36 ambazo nusu yake zilimuwezesha kumiliki kampuni yake mwenyewe ya kubuni na kutengeneza mavazi ya asili na magauni ya harusi iitwayo Nandy African Print.
Ilikuwa atoke kwa Akili the Brain?
Kipaji chake kilikuwa kitoke kwa mara ya kwanza Akili Records chini ya Akili The Brain. Nandy anasema kuwa katika kuhangaika kwake kutoka kimuziki alishawahi kufika kwenye studio yake na kutengeneza ngoma nne lakini hazikufanikiwa kutoka mpaka alipopata shavu la kwenda Nigeria kwenye Karaoke ya Tecno

BARAKA DA PRINCE AJITOA ROCKSTAR 4000 YA ALIKIBA, ATAJA SABABU

Mwimbaji maarufu wa muziki Bongo, Baraka Da Prince aliyesaini mkataba wa kufanya kazi na label ya Rockstar 4000 mwaka jana 2016, ameamua kuachana na lebo hiyo huku akibainisha sababu za kufanya maamuzi hayo magumu.
Akizungumza leo Julai 21, 2017 kupitia kipindi cha XXLBaraka amethibitisha kuwa hayupo tena chini ya Rockstar4000 na kuwa anafanya kazi zake binafsi akidai kuna mambo hayapo sawa kati yake na menejimenti huku akisisitiza siyo kwa sababu Alikiba amekuwa mmoja wa wakurugenzi wa label hiyo.
”Kuna vitu lazima uvihoji na ukiona watu unaofanya nao kazi kama kampuni wanakuwa hawajali kitu unachotaka kufahamu kuhusu makubaliano yenu ya kazi inakuwa na mashaka kidogo”
“Naweza kusema sipo chini ya Rockstar kwa sababu mimi ndio boss wa muziki wangu, mimi ndio nafanya kazi, kukiwa na vitu havipo sawa kwa upande wangu mimi ndio naweza kutoa kauli ya mwisho, sipo chini ya Rockstaar
“Kuna vitu haviko sawa hilo neno boss zito sana, unaponiambia mtu ni boss wangu, how? Boss kivipi kwangu? Alikiba kuwa director wa Rockstar mimi ndio nijitoe, hapana…. kuna vitu havipo sawa na uongozi wa Rockstar
“Nilipokwenda Rockstar4000 sikusaini chini ya AliKiba, mimi nina matatizo binafsi na uongozi na kama mambo hayapo sawa ukiona kitu jua kipo chini ya Baraka,” alisema Baraka the Prince.

Mesen: Mastaa ‘Wameniliza’ Sana!

RE
PRODYUZA wa Ngoma ya Hainaga Ushemeji ya Man Fongo, Jerry Boniphace ‘Mesen Selekta’ amesema kuwa, mastaa kibao wa Bongo Fleva aliokuwa akiwatengenezea ngoma wamemliza sana kwa kumlipa mkwanja kiduchu na wengine bure kabisa na kumsababishia kujikita kwenye muziki.
Akibonga na Over Ze Weekend, Mesen anayebamba na Ngoma ya Sukari akiwa chini ya Kampuni ya Dadid Investment alisema, kwa muda mrefu amekuwa akiwarekodia mastaa lakini kipato kiduchu alichokuwa akilipwa huku wengine wakitanguliza ushkaji kutokana na kazi hiyo aliokuwa akiwafanyia imemfanya kuwakimbia.
“Nimeona bora akili yangu ijikite zaidi katika kuimba japo nilikuwa sipo sana. Sasa nipo kamili na mashabiki wategemee ngoma juu ya ngoma kwa mwaka huu,” alisema Mesen ambaye pia ni mmiliki wa Studio ya De Fatality Music.

Tuesday 4 August 2015

EXCLUSIVE: KAULI YA SNURA BAADA YA SHILOLE KUFUNGIWA MUZIKI IKO HAPA


Kama unakumbuka vizuri nyuma kidogo kuliwahi kuibuka na mchuano mkali kati ya Mwanadada Shilole pamoja na Snura Mushi, kwenye game la muziki hapa Tz, ikiwa kipindi hicho ‘Majanga‘ ya Snura ilikuwa imebamba na ‘Nakomaa na Jiji‘ ya Shilole  ilikuwa imebamba pia.

Uvumi ukasambaa sana kuwa Shilole na Snura wanabifu, ikaenda ikaendaaa mwishowe zikasambaa nyepesi nyepesi zingine kuwa Snura kamuinulia Shilolemikono, mara baada ya kuonekana amekaa kimya bila kutoa vitu.

Baada ya Snura kujifungua mtoto alirudi na wimbo wa ‘Hawashi na kujitetea kuwa ukimya wake ulisababishwa na ujauzito, sasa hivi anategemea kutoa Video mpya ya wimbo unaoitwa ‘Najidabua

Lakini hii ndio kauli aliyoitoa mara baada ya aliyedaiwa kuwa mpinzani wake maarufu kwa jina la Shilole a.k.aShishibaby or Mrs Nuh kufungiwa muziki na BASATA kwa muda wa mwaka mzima hapa anafunguka zaidi.

” Kwa kweli naamini kuwa Shilole ni mtu mzima kwa kilicho mtokea atakuwa amejifunza nini kinatakiwa na nini hakitakiwi kwenye muziki, nachokiamini mimi, Shilole hawezi kurudia tena makosa coz hilo ni pigo kali sana, ninacho waomba BASATAwangempunguzia adhabu ikabaki hata miezi mitatu au ikiwezekana wamsamehe kabisa” Amesema Snura

 

Mke Wa Bobby Brown Akimbizwa Hospitali Baada Kumuaga Bobbi Kristina


 

Mwanamuziki Bobby Brown amezidi kuumia baada ya kuzikwa jana mtoto wake Bobbi Kristina mwenye umri wa miaka 22 na mke wake anayeitwa Alicia Etheredge akikambizwa hospitali baada ya kuzimia.
Ripoti ya TMZ inaeleza, muda mchache baada ya kutoa heshima za mwisho na kuaga kwa Bobbi Kristina, mke wa Bobby Brown amabe juzi kati alijifungua mtoto anayeitwa Bodhi, aliingizwa kwenye gari la wagonjwa (Ambulance) na kukimbizwa hospitali.

 
Lakini, muda sio mrefu Alicia aliweza kurudi kwenye hali yake ya kawaida, Bobby anategemewa kufika kwenye maziko ya Bobbi ambayo yatafanyika New Jersey leo. Bobbi Kristina amefanyiwa misa katika kanisa la St. James United Methodist Church, kanisa alilokuwa akienda kusali na marehemu mama yake Whitney Houston inasemekana kwamba picha ya Whitney Houston ilikuwepo pale.

 
Waombolezaji walitoa mafuriko ya machozi wakati kwaya ikiimba wimbo wa “Stand” ulioimbwa na Donnie McClerkin, wimbo ambao uliimbwa pia wakati wa maziko ya mama yake miaka mitatu iliyopita.
Kwenye mazishi hayo ambayo yalikuwa yakiendelea vizuri, shangazi wa marehemu Bobbi Kristina, Leolah Brown aliombwa aondoke kanisa kufuatia ugomvi uliozuka wakati Pat Houston alipokuwa akitoa heshima za mwisho kwa Bobbi Kristina.

 
Akiongea na maripota nje ya kanisa, Leolah alilalamika kwamba “whitney Houston atakuwa akimfuata Pat Houston kutoka kaburini” kabla hajaenda kutoa heshima kwa marehemu kwa Bobbi Kristina ambaye alikuwa ndani ya jeneza la silva, akiwa anaonekana vry beautiful.

 
Bobbi Kristina alifariki Jumamosi baada ya kukutwa hajijui akiwa ameanguka bafuni kwenye bathtub mwezi Januari.

 
Hali hiyo ya kutojijua alikaa nayo kwa miezi sita, Mungu ailaze roho marehemu mahali pema peponi..Amen.

Hanscana “Ma-Director wengi wa bongo wanapenda umwinyi”


Director mdogo ambae anafanya vizuri kwa sasa katika game hii ya bongo kwa kufanya video kali na kupelekewa kukubaliwa na wasanii kibao na kutaka kufanya nae video amefunguka na kusema kwamba waongozaji wengi wa muziki hapa bongo wanapenda umwinyi.

Hanscana aliyasema hayo mara baada ya kueleza chance kubwa aliyo ipata wakati wa Director mkubwa kutoka Ghana “Justin Campos” kutimba bongo na kuwaelekeza jinsi yeye anavyofanya kazi na jinsi anavyo jituma licha ya kuwa ni mkubwa kwa maana ya kwamba anafanya vitu ambavyo kwa bongo wengi wamezoea kutumikisha wasaidizi wao na bila kuwapa ujuzi wowote.

Nuh mziwanda – Wema ameitengeneza hiyo Audio, Sio sauti yangu


Nuh mziwanda  amesema kuwa  sauti inayosikika kwenye audio iliyovuja akisikika akimtongoza wema sio yake, amedai hiyo audio imetengenezwa.

Akiongea na mtandao wa Bongo5 Nuh amemshutumu Wema na timu yake kwa kuamua kumchafua yeye na mpenzi wake shilole ambaye tayari wamepatana.

“Hili suala nalichukulia kawaida na naona ni ushamba na upu*vu ha hawana akili hata kidogo. Kama ni kweli angemfuata shishi akamwamba kwamba ‘mpenzi wako kafanya kitu Fulani Fulani kwangu’ sio kutangaza. Na kama kweli, kwanini asingesema wengine wanaomtongoza na akaweka mitandaoni? Ni wema na watu wake wote ndio wamefanya hivi! Siku ya kwanza shishi alilipokea vibaya  lakini baada ya kumuelewesha kanielewa.” Nuh alisema

Shilole amefunguka kuwa hana ugomvi na mtu na wala hajali kama wametengeneza au vipi kwasababu Nuhalishamuomba msamaha na wamesameheana.