ADSENSE FLOAT CENTER

Tuesday 4 August 2015

Nuh mziwanda – Wema ameitengeneza hiyo Audio, Sio sauti yangu


Nuh mziwanda  amesema kuwa  sauti inayosikika kwenye audio iliyovuja akisikika akimtongoza wema sio yake, amedai hiyo audio imetengenezwa.

Akiongea na mtandao wa Bongo5 Nuh amemshutumu Wema na timu yake kwa kuamua kumchafua yeye na mpenzi wake shilole ambaye tayari wamepatana.

“Hili suala nalichukulia kawaida na naona ni ushamba na upu*vu ha hawana akili hata kidogo. Kama ni kweli angemfuata shishi akamwamba kwamba ‘mpenzi wako kafanya kitu Fulani Fulani kwangu’ sio kutangaza. Na kama kweli, kwanini asingesema wengine wanaomtongoza na akaweka mitandaoni? Ni wema na watu wake wote ndio wamefanya hivi! Siku ya kwanza shishi alilipokea vibaya  lakini baada ya kumuelewesha kanielewa.” Nuh alisema

Shilole amefunguka kuwa hana ugomvi na mtu na wala hajali kama wametengeneza au vipi kwasababu Nuhalishamuomba msamaha na wamesameheana.

0 comments:

Post a Comment